Thursday, April 13, 2017

MH. MAKONDA ATEMBELEA UJENZI WA HOSPITALI CHANIKA

Mh Paul Makonda leo hii ametembelea ujenzi wa Hospitali ya Kinamama ya Chanika unaofadhiliwa na ubalozi wa Korea Kusini na kugharimu zaidi ya Tshs. 8.8 Bilioni uliokamilika kwa 90% hadi hivi sasa.
Mwanzoni 2016 Mh Makonda alipeleka maombi (propasal) ya kuomba washikadau wa maendeleo mbalimbali ikiwemo ubalozi wa Korea Kusini kusaidia katika ujenzi wa hospitali ya kisasa ya Mama na Mtoto , ambapo ubalozi huo ulikubali propasal hiyo
Ujenzi wa hospitali hiyo unaenda sambamba na ujenzi wa nyumba 28 ajili ya wauguzi na madaktari watakaohudumu hospitali hiyo masaa 24. Mpaka sasa 90% ya ujenzi huo imekamilika na kazi ya kufunga vitanda 160 vya wagonjwa na 10 vya kujifungulia na ufungaji wa vifaa vingine inaendelea kwa sasa.
Hospitali hii itakuwa ni mahususi kwa wakina mama na Watoto inatarajiwa kufunguliwa mwezi Juni mwaka huu (2017) na Mh Magufuli

No comments:

Post a Comment